Tuesday, November 1, 2016

KUMBE MUHAMMAD ALIKUWA MUISLAM WA KWANZA


UTATA MKUBWA KATIKA KORAN
NANI ALIKUWA MUISLAM WA KWANZA?
Ndugu zanguni:
Leo ningependa tuangalie kiundani kidogo kuhusu, “nani alikuwa Muislam wa Kwanza” kutokana na Koran iliyo teremshwa na Allah.
Kwa mujibu wa vifungu kadhaa katika Quran, Muhammad ni Muislamu kwanza :
Quran 6: 14. Sema: Je, nimchukue rafiki mlinzi asiye kuwa Mwenyezi Mungu, ambaye ndiye Muumba mbingu na ardhi, naye ndiye anaye lisha wala halishwi? Sema: Mimi nimeamrishwa niwe wa kwanza wa wenye kusilimu. Na wala kabisa usiwe miongoni wa washirikina.
Hana mshirika wake. Na hayo ndiyo niliyo amrishwa, na mimi ni wa kwanza wa Waislamu. (Wa ' Ana ' Awwalu Al- Muslimin ). S. 6:161-163
Sema (Ewe Muhammad): Hakika Mimi nimeamrishwa nimuabudu Mwenyezi Mungu, kwa kumsafishia Dini Yeye ( tu ). Na nimeamrishwa niwe wa kwanza wa wale ambao ni Waislamu ( kujisalimisha kwake ). S. 39:11-12 Pickthall
Je, nani alikuwa Muislamu wa Kwanza?
1. Katika Suran 6: 163 Koran inadai kuwa Muhammad ndie Muislam wa kwanza.
2. Katika S. 02:30 , 34-35 , 37 Koran inadai kwamba, ni Ibrahim na waumini walio zaliwa kabla ya Muhammad ndio walikuwa Waislam wa Kwanza.
3. Katika S. 5:110-111 Koran inadai kuwa eti Isa Bin Maryam ndie alikuwa Muislam wa kwanza.
4. Katika S. 2:37 Koran inadai kuwa eti Adam ndie aliye kuwa Muislam wa Kwanza.
SWALI NI HILI:
Nani alikuwa Muislam wa kwanza?
Kwanini Koran ifanye makosa makubwa namna hii na kudai eti Muhammad ndie alikuwa Muislam wa Kwanza?
Waislam wanaweza kudai kuwa kila umma ulitumiwa nabii.
Kama hayo madai ni kweli, basi maswali haya yanahitaji majibu:
1. Nani ni Nabii wa Waafrika?
2. Nani ni Nabii wa Wazungu?
3. Nani ni Nabii wa Wamarekani?
4. Nani ni Nabii wa Wachina?
HAKIKA KUNA UTATA MKUBWA SANA KATIKA KORAN YA ALLAH ILIYO SHINDWA KUTUELEZA NI NANI ALIKUWA MUISLAM WA KWANZA.
Ndugu yangu,
Karibu kwa Yesu Kristo aliye kuja kwa Mataifa Yote.
Matayo 28: 18 Yesu akaja kwao, akasema nao, akawaambia, Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani.
19 Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu;
20 na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari.
Yesu Kristo alikuwa kwa Mataifa yote kama Injili kutokana na Matayo inavyo sema hapo juu. Hakika Msamaha wa dhambi unapatikana kupitia Yesu pekee. Soma: Luka 7 48 Kisha Yesu alimwambia mwanamke, Umesamehewa dhambi zako.
KARIBU SANA KWA YESU KRISTO ALIYE HAI.
Mungu awabairiki sana
Katika Huduma Yake
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.
Copyright © Max Shimba Ministries

No comments:

WHY CHRISTIANITY IS BETTER THAN ISLAM?

Has Islam Improved to Become Better Than Christianity? Does Muhammad fulfill and complete the mission and purpose of Christ? Muhammad emphat...

TRENDING NOW